Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Ad-Dhuhâ

93 – WADH-DHUH’AA

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. Naapakwamchana! 
  2. 2. Nakwausiku unapo tanda! 
  3. 3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
  4. 4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
  5. 5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
  6. 6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
  7. 7. Na akakukuta umepotea akakuongoa?
  8. 8. Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
  9. 9. Basi yatima usimwonee!
  10. 10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
  11. 11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.