Quran in Swahili
Al-Aʽlâ
87 – AL – AA’LAA
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
- 1. Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
- 2. Aliye umba, na akaweka sawa,
- 3. Na ambaye amekadirianaakaongoa,
- 4. Na aliye otesha malisho,
- 5. Kisha akayafanya makavu, meusi.
- 6. Tutakusomesha wala hutasahau,
- 7. Ilaakipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahirina yaliyo fichikana.
- 8. Na tutakusahilishia yawe mepesi.
- 9. Basi kumbusha,kamakukumbusha kunafaa.
- 10. Atakumbuka mwenye kuogopa.
- 11. Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
- 12. Ambaye atauingia Moto mkubwa.
- 13. Tena humo hatakufa wala hawi hai.
- 14. Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
- 15. Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
- 16. Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
- 17. Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
- 18. Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
- 19. Vitabu vya Ibrahimu na Musa.