Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Al-Balad

90 – AL – BALAD

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. NaapakwaMji huu! 
  2. 2. Nawe unaukaa Mji huu.
  3. 3. Na naapakwamzazi na alicho kizaa. 
  4. 4. Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
  5. 5. Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
  6. 6. Anasema: Nimeteketeza chungu yamali.
  7. 7. Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
  8. 8. Kwani hatukumpa macho mawili?
  9. 9. Na ulimi, na midomo miwili?
  10. 10. Na tukambainishia zote njia mbili?
  11. 11. Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
  12. 12. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
  13. 13. Kumkomboa mtumwa;
  14. 14. Au kumlisha siku ya njaa
  15. 15. Yatima aliye jamaa,
  16. 16. Au masikini aliye vumbini.
  17. 17. Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
  18. 18. Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
  19. 19. Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
  20. 20. Juuyaoutakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.