Quran in Swahili
Al-Burûj
85 – AL – BURUUJ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
- 1. Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
- 2. Na kwa siku iliyo ahidiwa!
- 3. Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
- 4. Wameangamizwa watu wa makhandaki
- 5. Yenye moto wenye kuni nyingi,
- 6. Walipo kuwa wamekaa hapo,
- 7. Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
- 8. Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
- 9. Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
- 10. Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
- 11. Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenyemitoipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
- 12. Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
- 13. Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
- 14. Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
- 15. Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
- 16. Atendaye ayatakayo.
- 17. Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
- 18. Ya Firauni na Thamudi?
- 19. Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
- 20. Na Mwenyezi Mungu nyumayao
- 21.Balihii ni Qur’ani tukufu
- 22. Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.