Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Al-Infitâr

82 – AL – INFIT’AAR

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. Mbingu itapo chanika,
  2. 2. Na nyota zitapo tawanyika,
  3. 3. Na bahari zitakapo pasuliwa,
  4. 4. Na makaburi yatapo fukuliwa,
  5. 5. Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza,nailicho bakisha nyuma. 
  6. 6. Ewe mwanaadamu!Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
  7. 7. Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
  8. 8. Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
  9. 9. Sivyo hivyo!Balinyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo. 
  10. 10. Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
  11. 11. Waandishi wenye hishima,
  12. 12. Wanayajua mnayo yatenda.
  13. 13. Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
  14. 14. Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
  15. 15. Wataingia humo Siku ya Malipo.
  16. 16. Na hawatoacha kuwamo humo.
  17. 17. Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
  18. 18. Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
  19. 19. Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.