Quran in Swahili
Al-Layl
92 – AL – LAYL
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
- 1. Naapakwausiku unapo funika!
- 2. Na mchana unapo dhihiri!
- 3. NakwaAliye umba dume na jike!
- 4. Hakika juhudi zenu bila ya shakanimbali mbali.
- 5. Ama mwenye kutoanaakamchamngu,
- 6. Na akaliwafiki lilio jema,
- 7. Tutamsahilishia yawe mepesi.
- 8. Na ama mwenye kufanya ubakhili,na asiwe nahaja ya wenzake,
- 9. Na akakanusha lilio jema,
- 10. Tutamsahilishia yawe mazito!
- 11. Namaliyake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
- 12. Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
- 13. Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
- 14. Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
- 15. Hatauingia ila mwovu kabisa!
- 16. Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
- 17. Na mchamngu ataepushwa nao,
- 18. Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
- 19. Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
- 20. Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
- 21. Naye atakuja ridhika!