Quran in Swahili
Al-Maʽârij
70 – AL – MAA’RIJ
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
- 1. Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
- 2. Kwa makafiri – ambayo hapana awezaye kuizuia –
- 3. KutokakwaMwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
- 4. MalaikanaRoho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
- 5. Basi subirikwasubira njema.
- 6. Hakika wao wanaiona iko mbali,
- 7. Na Sisi tunaiona iko karibu.
- 8. Siku ambayo mbingu zitakapo kuwakamamaadeni iliyo yayushwa.
- 9. Na milima itakuwakama
- 10. Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
- 11. Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
- 12. Na mkewe, na nduguye,
- 13. Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
- 14. Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
- 15. La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
- 16. Unao babua ngozi ya kichwa!
- 17. Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
- 18. Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
- 19. Hakika mtu ameumbwa na papara.
- 20. Inapo mgusa shari hupapatika.
- 21. Na inapo mgusa kheri huizuilia.
- 22. Isipo kuwa wanao sali,
- 23. Ambao wanadumisha Sala zao,
- 24. Na ambao katikamaliyao iko haki maalumu
- 25. Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
- 26. Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
- 27. Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
- 28. Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
- 29. Na ambao wanahifadhi tupu zao.
- 30. Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi –
- 31. Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
- 32. Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
- 33. Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
- 34. Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
- 35. Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
- 36. Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
- 37. Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
- 38. Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
- 39. La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
- 40. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
- 41. Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
- 42. Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
- 43. Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
- 44. Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.