Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Al-Mâʽûn

107 – AL – MAAU’N

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. Je!Umemwona anaye kadhibisha Malipo?
  2. 2. Huyo ndiye anaye msukuma yatima,
  3. 3. Wala hahimizi kumlisha masikini.
  4. 4. Basi, ole wao wanao sali,
  5. 5. Ambao wanapuuza Sala zao;
  6. 6. Ambao wanajionyesha,
  7. 7. Nao huku wanazuia msaada.