Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Al-Qâriʽah

101 – AL – QAARIA’H

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.  

 

  1. 1. Inayo gonga!
  2. 2. Nini Inayo gonga?
  3. 3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
  4. 4. Siku ambayo watu watakuwakamanondo walio tawanyika; 
  5. 5. Na milima itakuwakamasufi zilizo chambuliwa! 
  6. 6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
  7. 7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
  8. 8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
  9. 9. Huyo maskani yake yatakuwa MotowaHawiya! 
  10. 10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
  11. 11. Ni Moto mkali!