Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Al-Sharh

94 – ASH-SHARH’

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. Hatukukunjulia kifua chako?
  2. 2. Na tukakuondolea mzigo wako,
  3. 3. Ulio vunja mgongo wako?
  4. 4. Na tukakunyanyulia utajo wako?
  5. 5. Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
  6. 6. Hakika pamojanauzito upo wepesi. 
  7. 7. Na ukipata faragha, fanya juhudi.
  8. 8. Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.