Quran translations in many languages

Quran in Swahili

Al-Zalzalah

99 – AZ-ZILZALAH

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. Itakapo tetemeshwa ardhikwamtetemeko wake! 
  2. 2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
  3. 3. Na mtu akasema: Ina nini?
  4. 4. Siku hiyo itahadithia khabari zake.
  5. 5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
  6. 6. Siku hiyo watu watatokakwamfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! 
  7. 7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
  8. 8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!