Quran translations in many languages

Quran in Swahili

At-Tîn

95 – AT-TIN

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

  1. 1. Naapa kwa tini na zaituni!
  2. 2. Na kwa Mlima wa Sinai!
  3. 3. Na kwa mji huu wenye amani!
  4. 4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
  5. 5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
  6. 6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
  7. 7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
  8. 8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?